Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir,amesema kuwa jeshi limetibua njama ya mapinduzi dhidi ya serikali yake.
Rais Kiir amewalaumu wanajeshi wanaomuunga mkono aliyekuwa naibu wake Riek Machar ambaye alifutwa kazi, kwa mapigano yaliyozuka kati ya wanajeshi wake Jumapili usiku. Amesema kuwa serikali sasa imedhibiti hali.
Wanajeshi mahasimu, walipigana vikali kwa masaa kadhaa na inaarifiwa kuna majeruhi kadhaa huku mamia wakitoroka mji wa Juba..Kiongea na waandishi wa habari, Bwana Kiir alisema serikali imedhibiti hali huku ikitangaza sheria ya kutotoka nje nyakati za usiku.
Kwa sasa milio ya risasi imekwisha. Kumekuwa na hali ya taharuki nchini Sudan Kusini tangu mwezi Julai wakati Rais Kiir alipowafuta kazi mawaziri wake akiwemo bwana Machar.
Wito wa utulivu
Awali Umoja wa Mataifa ulitoa wito wa utulivu nchini Sudan Kusini baada
Post a Comment