http://tropicalpoultryfarming.blogspot.com/

MAN UNITED WATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA LIGI, SPURS NJE

KOCHA David Moyes ameendelea kupambana baada ya jana kuiongoza Manchester United kushinda mabao 2-0 dhidi ya Stoke City katika Kombe la Ligi England.
Ushindi huo wa United jana ulitokana na mabao ya Ashley Young dakika ya 61 na Patrice Evra dakika ya 78. 

Raha ya bao: Ashley Young (kushoto) akishangilia baada ya kuifungia Manchester United bao la kwanza dhidi ya Stoke City

Katika mchezo mwingine, mshambuliaji Emmanuel Adebayor alirejea uwanjani na kufunga bao moja wakati timu yake, Tottenham Hotspur ikifungwa 2-1 na West Ham United, mabao ya 
Jarvis dakika ya 80 na Maiga dakika ya 85.
Man United sasa itamenyana na Sunderland katika Nusu Fainali ya michuano hiyo maarufu kama Capital One, wakati West Ham itakipiga na Manchester City. 
Adebayor akishangilia bao lake ambalo hata hivyo halikuweza kuinusuru Spurs na kipigo 

Nayo Manchester City iliifunga 3-1 Leicester na kufikisha jumla ya mabao 75 katka michezo 25

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

CHARLES CHAMI. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget