http://tropicalpoultryfarming.blogspot.com/

WANA LAMBALAMBA WA AZAM FC WAJIULIZA MBELE YA JKT RUVU LEO PALE AZAM COMPLEX


Katika mchezo wa kwanza uliofanyika kwenye uwanja huohuo wa Azam Complex Azam walilala kwa bao 1-0 mbele ya vijana wa kocha Fredy Minziro kitu ambacho kinaashiria ugumu wa mchezo

MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Tanzania bara, Azam FC,   leo Jumamosi, wanatarajia kushuka kwenye dimba lao la Azam Complex kuwakabili Maafande wa JKT Ruvu, kutoka mkoani Pwani.
Azam ambao Jumamosi iliyopita waliondoshwa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na El Merreikh, bila shaka itaingia katika mchzo huo ikiwa na hasira za kutaka kupoza machungu yake na kupunguza idadi ya pointi kati yao na vinara wa ligi hiyo Yanga.
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika kwenye uwanja huohuo wa Azam Complex Azam walilala kwa bao 1-0 mbele ya vijana wa kocha Fredy Minziro kitu ambacho kinaashiria ugumu wa mchezo huo wa kesho.
Kabla ya kutolewa na El Merreikh kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika Azam ilicheza mechi mbili za ligi dhidi ya Ruvu Shooting na Tanzania Prisons na zote ilipata sare ya bila kufungana huku JKT Ruvu nayo ikienda sre ya 1-1 na Tanzania Prisons Jumamosi iliyopita kwenye uwanja huo wa Azam Complex.
Kocha wa muda George Nsimbe ‘Besti’ huo utakuwa mtihani wake wa kwanza kukiongoza kikosi cha Azam akiwa mkuu wa benchi la ufundi baada ya kukabidhiwa mikoba hiyo Jumatatu ya wiki hii kufuatia kutimuliwa kwa kocha mkuu Joseph Omog.
Nsimbe atahakikisha anatumia silaha zote muhimu kwa ajili ya kupata ushindi katika mchezo huo ili kurudisha matumaini ya timu hiyo kutetea ubingwa wao wa ligi ya Vodacom ili kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani.
Kwaupande wao JKT Ruvu waliopo kwenye nafasi ya 10, watahakikisha wanapambana na kupata ushindi ili kujinasua na janga la kushuka daraja msimu huu.
Washambuliaji Idd Mbaga Reliants Lusajo na Amosi Mgisa watakuwa na kazi moja tu ya kulitia msukosuko lango la Azam ambalo asilimia kubwa ya wachezaji wake wanaonekana kutokuwa sawa baada ya ndoto zao kupotea katika michuano ya ligi ya Mabingwa Afrika.
Bilashaka kocha Nsimbe atataka kumpumzisha kipa wake chipukizi Aishi Manula kwenye mchezo huo na kumtumia mkongwe, Mwadin Ali huku akiendelea kuwatumia washambuliaji wake Didier Kavumbagu, Kipre Tchetche ambao wameonyesha uelewano mkubwa msimu huu sambamba na wingi Brian Majwega.
Pamoja na kuhakikishiwa kibarua chake na uongozi wa timu ya Azam lakini faraja pekee kwa kocha George Nsimbe ni kupata pointi tatu ambazo zitairudisha timu hiyo katika mbio za kutetea ubingwa na kuitia wasiwasi Yanga inayoongoza ligi hiyo kwa sasa.

Labels:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

CHARLES CHAMI. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget