http://tropicalpoultryfarming.blogspot.com/

A.J.T.C WAPATA SERIKALI YA WANAFUNZI BAADA YA MWAKA MMOJA NA NUSU, KWA UCHAGUZI WA KIDEMOKRASIA.

wapiga kura wakiwa katika foleni wakisubiria kupiga kura (picha na charles chami)
Baaba ya mwaka mmoja na nusu kutokuwa na serekali ya wanafunzi chuo cha uandishi wa habari na utangazaji arusha kimepata serikali   mpya  baada ya kufanyika uchaguzi wa kidemokrasia mapema leo chuoni hapo.

Wanafunzi wa chuo hicho wamejitokeza kwa wingi katika  kituo cha kupiga kura na kupata haki yao ya msingi ya kumchaguwa kiongozi wanaemtaka atakaewaongoza kwa kwa kipindi cha mwaka mmoja
Mbele ni Bwana Agape msumari  akiwa anaitumia haki yake ya msingi ya kupiga kura (picha na charles chami)
Nafasi ambazo zilikuwa zikwaniwa ni pamoja na nafasi ya afisa mausiano (P.R.O), Katibu, Makamu wa raisi  na Raisi ambapo katika nafasi ya ukatibu ilikuwa inawaniwa na Inocent Bambara ambae amepata kura 48, Bogoma wa Bugoma kura 80 na Haji Juma kura 126 kati ya wapiga kura 256 waliojitokeza kupiga kura

Haji Juma katibu wa AJTC (picha na charles chami)
Nafasi  nyingine zilizokuwa zikiwaniwa ni Afisa mausiano (P.R.O) Wagombea walikuwa wawili ambao ni Benjamin Jocob alimarufu kama (Big shop beny) aliepata kura 71 na Protte Proffit Mmanga kura 135
Protte Profit Mmanga P.R.O wa AJTC (picha na charles chami)
Katika nafasi ya makamu wa raisi ilikuwa na wagombea wane ambao ni Baraka Charles kura 52, Ruthibetha Fransis kura 77, Robson Jackson kura 31 na Emma moshi kura 93 na kura zilizo aribika zikiwa ni 3 kati ya wapiga kura 256

Emma moshi makamu wa raisi katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji arusha (picha na charles chami)
Nafasi ya mwisho ambayo ilikuwa ikiwaniwa ni nafasi ya Uraisi ambapo wagombea walikuwa ni wawili waliojitokeza ambao ni Hababi Mohamed kura 64 na na  Kephasi Daniel Ilani ambae ameibuka kudedea kwa jumla ya kura 191 na kura moja kuaribika kati ya 256 zilizopigwa.

Bwana Kephas Daniel Illani Raisi wa A.J.T.C 2015-216(picha na charles chami)
JUMLA YA WA WASSHINDI PAMOJA NA KURA ZAO
Jina la mgambea
Jumla ya wapiga kura
Kura  alizopata
Kura zilizo aribika
Nafasi

KEPHASI DANIEL

256

191

1

RAISI

EMMA MOSHI

256

93

3
MAKAMU WA RAISI
PROTTE .P.
MMANGA

256

135

HAMNA

P.R.O

HAJI JUMA

256

126

HAMNA

KATIBU

Hii inakuwa ni serikali ya nane ya wanafunzi wa chuo hiki baada kukaa takribani mwaka mmoja na nusu bila serikali, huku ikitanguliwa na serikali mbili za mwisho ambazo zilikuwa na maswaibu mengi ambazo zilipelekea kuvunjika kwa serikali hizo
Serikali iliyopita iliyokuwa inaongozwa na raisi George silange  ambayo inasemekana ndo serikali iliyokaa madarakani kwa muda mfupi na kuvunjika kutokana na serikali yake kutofautiana na uongozi wa juu wa chuo kwenye mchakato wa kutengeneza katiba ya chuo hicho kitendo ambacho kilimfanya Silange  ajiuzulu kuwa raisi wa A.J.T.C.
George silange raisi wa serikali iliyopita ya AJTC (picha na maktaba)
Alikadhalika kabla ya serikali hiyo ya silange kulikuwepo na serikali nyingine iliyovunjika iliyokuwa chini ya David Adriano Ambapo uongozi wake ulichukuwa uamuzi wa kuandaa tamasha bila idhini ya chuo kitendo ambacho kilipelekea kuvunjwa kwa serikali yake

David Adriano raisi wa serikali iyovunjika kabla ya George silange (picha na maktaba)
Serikali hii mpya ya bwana Illani inatabiriwa kuwa serikali ya amani na inayo fuata ueledi wa uongozi kutokana na aina ya viongozi waliochaguliwa.  Raisi huyo mpya  anatarajia kuwasilisha baraza lake la mawaziri siku ya jumatatu ya tarehe 16 na uongozi wake utakula kiapo siku ya jumanne.

Labels:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

CHARLES CHAMI. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget