http://tropicalpoultryfarming.blogspot.com/

LIGI KUU ENGLAND YAREJEA DIMBANI KUANZIA DABI YA MERSEYSIDE!!


MERSEYSIDE_DABI

NANI KIDEDEA DABI ya MERSEYSIDE ambayo itakuwa Dabi ya 221?
Hili ni swali gumu sana kulijibu.
Kwa Misimu miwili iliyopita, Everton wamekuwa wakimaliza Ligi Kuu England wakiwa juu ya wapinzani wao wa Jadi, Liverpool, lakini katika Mechi 4 walizocheza Everton hawakuifunga Liverpool hata Mechi moja kwa kutoka Sare 2 na Kufungwa 2.
Msimu huu, Liverpool wameanza kwa moto, wako Nafasi ya Pili, wameshinda Mechi 7 na wako Pointi 3 mbele ya Everton walio Nafasi ya 6 na wameshinda Mechi 5.
Hali hii ya Liverpool imesaidiwa sana na ushirikiano wa Mastraika wao Luis Suarez na Daniel Sturridge ambao kati yao wamefunga Jumla ya Mabao 21.
Everton, Msimu huu, hawajafungwa kwao Goodison Park na ngome yao ni ngumu kufungika wakiwa wametoka Mechi 6 kati ya 11 za Ligi bila kupigwa hata Bao moja.
ARSENAL v SOUTHAMPTON



WALCOTT_WILSHERE_OX
-Emirates Stadium [Jumamosi Saa 12 Jioni]
Hii ni Mechi ambayo, hadi sasa Difensi ngumu kwenye Ligi, inakutana na Arsenal ambayo imepiga Bao katika Mechi 15 za Ligi mfululizo hadi Mabingwa Manchester United walipoichapa Arsenal Bao 1-0 katika Mechi yao ya mwisho ya Ligi Kuu England.
Msimu huu, Southampton wamefungwa Bao 5 tu lakini wanarudi Uwanja wa Emirates ambao Msimu uliopita walitwangwa Bao 6-1.
Safari hii, Arsenal wataimarika kwa kurudi dimbani kutoka Majeruhi kulomweka Miezi miwili nje Mchezaji wa zamani wa Southampton, Theo Walcott, kama ilivyothibitishwa na Meneja Arsene Wenger.
FULHAM v SWANSEA
-Craven Cottage [Jumamosi Saa 12 Jioni]
Hii ni ‘lala salama’ kwa Meneja wa Fulham, Martin Jol, ambae anajua fika amekalia kuti kavubaada kupigwa Mechi 3 mfululizo za Ligi na tayari Klabu hiyo imechukua hatua kudhibiti hali yao mbaya kwa kumwajiri Kocha Mkuu wa zamani wa Man United Rene Meulensteen ambae Wadau wanahisi huyu ndio atakuwa ‘Meneja mpya!’
HULL v CRYSTAL PALACE
-KC Stadium [Jumamosi Saa 12 Jioni]
Mara ya mwisho kwa Hull City kuifunga Crystal Palace kwenye KC Stadium ilikuwa Mwaka 2008 wakati Timu zote zilipokuwa Daraja la Championship na tangu wakati huo Crystal Palace imeshinda mara 2 na Sare 4.
Lakini Hull City, Msimu huu, hawajafungwa kwao wakati Palace walichapwa Mechi 7 mfululizo hadi Mechi yao ya mwisho walipotoka Sare na Everton.
NEWCASTLE v NORWICH
-St James’ Park [Jumamosi Saa 12 Jioni]
Ni miaka 25 imepita tangu Norwich City waifunge Newcastle Uwanja wa St James’ Park lakini Norwich hii inavujisha Magoli kwani washapigwa Bao 21 kitu ambacho Meneja wao Chris Hughton itabidi akitilie mkazo sana.
Msimu huu, Newcastle, chini ya Alan Pardew, wamefungwa mara moja tu wakiwa Uwanja wao na wanatinga Mechi hii wakiwa wameshinda Mechi mbili za Ligi mfululizo.
STOKE v SUNDERLAND
Britannia Stadium [Jumamosi Saa 12 Jioni]
Ni Mechi inayokutanisha Timu ambazo zinasuasua huku Stoke City wakiwa hawajashinda Uwanjani kwao tangu Mechi yao ya pili ya Ligi Msimu huu na Sunderland wakiwa hawajashinda Ugenini kwenye Ligi tangu Mwezi Aprili.
Lakini hivi sasa Timu hizi zinaingia kwenye mabadiliko kwani Stoke City, chini ya Meneja Mark Hughes,  imetoka Sare Mechi mbili mfululizo na Sunderland, chini ya Gus Poyet, iliifunga Man City katika Mechi yao ya mwisho.
WEST HAM v CHELSEA

-Upton Park [Jumamosi Saa 2 na Nusu Usiku]
Mwaka mmoja uliopita, Carlton Cole alifunga Bao ambalo liliiwezesha West Ham kuichapa Chelsea Bao 3-1 ukiwa ni ushindi wao wa kwanza dhidi ya Chelsea tangu Mwaka 2003.
Baada ya hapo Cole aliihama Klabu hiyo lakini sasa amerudi tena na Chelsea nao wamemrudisha Kocha wao wa zamani Jose Mourinho ambae bado anasuasua kwenye Ligi na katika Mechi yao ya mwisho walitoka Sare 2-2 huko Stamford Bridge na West Brom na kunusurika kwa Penati ya utata.
MANCHESTER CITY v TOTTENHAM
-Etihad Stadium [Jumapili Saa 10 na Nusu Jioni]
Timu zote hizi zinatinga kwenye Mechi hii wakitokea kwenye vipigo vya kutia uchungu baada City kufungwa na Sunderland Bao 1-0 na Tottenham kutunguliwa pia 1-0 na Newcastle.
City hawajafungwa kwao Msimu huu lakini Spurs wameshashinda Mechi 3 Ugenini Msimu huu.
CARDIFF CITY v MANCHESTER UNITED
Cardiff City Stadium [Jumapili Saa 1 Usiku]
RVP_ROONEY_CLEVERLY
Man United wanategemea Nyota wao Robin van Persie, ambae ndie alifunga Bao la ushindi walipoichapa Arsenal Bao 1-0 katika Mechi yao ya mwisho ya Ligi, atakuwa fiti baada kushindwa kuiwakilisha Nchi yake Netherlands kwenye Mechi za Kimataifa kutokana na maumivu ya kidole cha Mguuni pamoja na Nyonga.
Lakini Man United itawakosa Michael Carrick na Phil Jones ambao wameumia na hivyo kulazimika kuwachezesha kwenye Kiungo Anderson, Tom Cleverley na Ryan Giggs huko Wales ambako hawajakutana na Cardiff City tangu Mwaka 1974 walipoifunga Bao 1-0.
Tegemeo kubwa la Cardiff kwa Magoli ni Kijana wa zamani wa Man United, Fraizer Campbell, ambae hajafunga kwenye Ligi tangu Mwezi Agosti ambapo Bao zake 2 ziliiua Man City.
WEST BROM v ASTON VILLA
The Hawthorns [Jumatatu Saa 5 Usiku]
Mara ya mwisho Timu hizi kukutana na Mshindi kupatikana ni Oktoba 2011 wakati West Brom ilipoifunga Aston Villa Bao 2-1 Uwanjani Villa Park.
Lakini tangu hapo, Dakika 270 za Soka zimepita bila mbabe kupatikana na wakati huu Timu zote zinafanya vyema kwenye Ligi huku WBA ikiwa imetoka kwenye Mechi iliyozua utata baada ya nusura kuichapa Chelsea Bao 2-1 Uwanjani Stamford Bridge kama si Penati ya utata ya Dakika ya mwisho ya 94 kuipa Chelsea Bao la kusawazisha.

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

CHARLES CHAMI. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget