http://tropicalpoultryfarming.blogspot.com/

TETESI ZA USAJILI ULAYA MBAPPE MBIONI KUJIUNGA NA PSG, COUTINHO BASI TENA

Philippe Coutinho sasa haiwezekani kujiunga na Barcelona akitokea Liverpool msimu huu wa majira ya joto kwa mujibu wa RAC1 kupitia Mundo Deportivo .
Madau kadhaa ya Barcelona kwa ajili ya mchezaji huyo yamekataliwa na klabu ya Liverpool imesisitiza Mbrazili huyo hauzwi.
Valencia wanakaribia kumsajili kwa mkataba wa mkopo kiungo wa Manchester United Andreas Pereira, kwa mujibu wa  Cadena Ser Valencia .
Pereira alikuwa Granada msimu uliopita na yupo mbioni kurudi kwenye La Liga msimu huu tena.
Kiungo wa Nice Jean-Michael Seri amefikia makubaliano ya mkataba wa miaka minne kujiunga na Barcelona, kwa mujibu wa  L'Equipe.
Bayern Munich wanaangalia uwezekan wa kumsajili mshambuliaji wa Paris Saint-Germain Julian Draxler, kwa mujibu wa  Westdeutsche Allgemeine Zeitung .
Mustakabali wa Drazxler PSG haueleweki kufuatia usajili wa Neymar, na Mjerumani huyo amehusishwana tetesi za kutaka kutua Arsenal, Liverpool na Manchester United.
Arsenal wamempa mkataba mpya wa miaka minne Alex Oxlade-Chamberlain wenye thamani ya paundi 125,000 kwa wiki kumzuia kwenda Chelsea, kwa mujibu wa  Daily Star .
Kylian Mbappe ameachwa kwenye mazoezi ya Monaco baada ya kufanya mabishano na Andrea Raggi Jumanne iliyopita kwa mujibu wa   L'Equipe .
Arsenal wamemtoa Jack Wilshere kwa AC Mila, limeripoti  Corriere dello Sport .
Wilshere amehusishwa na tetesi za kujiunga na klabu hiyo ya Serie A siku za nyuma, lakini mchezaji huyo anasita kuondoka Ligi Kuu Uingereza.
Manchester City itaendelea kumfukuzia Alexis Sanchez hadi mwisho wa dirisha la uhamisho, na wameandaa kitita cha paundi milioni 70 kwa ajili ya nyota huyo wa Arsenal, limeripoti Mirror .
Chelsea wanajipanga kutumia paundi milioni 200 kusajili wachezaji wapya watano ili kutimiza anachokitaka Antonio Conte, kwa mujibu wa Express .
Wachezaji watatu wa Southampton Virgil van Dijk, Cedric Soares na Ryan Bertrand wapo kwenye orodha ya wachezaji anaowataka Conte, kadhalika Danny Drinkwater wa Leicester City na kiungo wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain.
Nyota wa Paris Saint-Germain Julian Draxler anawaniwa na klabu za Uingereza, Man United, Arsenal na Liverpool ikiwa ataondoka Parc des Princes, kwa mujibu wa  Mirror .
Atletico Madrid imekubali kuilipa Chelsea €55 millioni kwa ajili ya kumnunua Diego Costa, kwa mujibu wa habari.
Costa kwa sasa yupo Brazili baada ya kukataa kurejea Chelsea na klabu pekee anayoitaka kujiunga nayo kwa sasa ni Atletico Madrid.
Liverpool wamekubali kufanya mkutano wa mwisho na Barcelona kuhusu uhamisho wa Philippe Coutinho, kwa mujibu wa Sport .
Klabu hiyo ya Ligi Kuu Uingereza imekataa ofa tele kwa ajili ya mchezaji huyo, ofa ya mwisho ilikuwa euro milioni 125. 
PSG wapo mbioni kutangaza usajili wa Kylian Mbappe kutoka Monaco, kwa mujibu wa habari kutoka  Mundo Deportivo .
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 atakuwa mchezaji wa pili ghali zaidi katika historia, baada ya klabu hiyo ya Paris kumsajili Neymar kwa euro milioni 222.
Real Madrid inataka kumtunuku Marco Asensio mkataba mpya hadi 2023 na kuiongeza bei yake hadi euro mlioni 500, kwa mujibu wa Marca .
Barcelona wametoa ofa ya euro milioni 30 kwa ajili ya kiungo wa Nice Jean Michael Seri katika harakati zao za kutafuta wachezaji wapya, limedai Sport.
Real Madrid imekataa ofa ya euro milioni 75 kwa ajili ya Mateo Kovacic kutoka Juventus, kwa mujibu wa AS .
West Brom wanafikiria kumsajli beki wa Liverpool Mamadou Sakho baada ya Manchester City kuonesha nia ya kumsajili Jonny Evans, kwa mujibu wa BBC .
Sakho anakadiriwa kuwa na thamani ya £30 millioni na Liverpool na aling'ara alipokuwa akitumika kwa mkopo Crystal Palace msimu uliopita baada ya kukataa kujiunga na West Brom.
Real Madrid wanajipanga kutoa dau la paundi milioni 46 kwa ajili ya kipa nambari moja wa Manchester United, David De Gea kwa mujibu wa  The Sun .
Inter imefanya jaribio la kumsajili beki wa Arsenal Shkodran Mustafi kwa uhamisho wa mkopo, kwa mujibu wa GIanlucaDiMarzio.com .
Miamba hao wa Serie A wanataka kuimarisha safu yao ya ulinzi na wanaamini Mjerumani huyo atakuwa suluhisho lao baada ya kumkosa Eliaquim Mangala kutoka Manchester City.
Chelsea watalazimika kukubali fedha kichele katika ofa ya Diego Costa tofauti na ile waliyotarajia wangeipata kwa biashara ya mchezaji huyo, kwa mujibu wa  Sun .
Costa amekuwa tu kama mchezaji wa ziada Darajani, na tetesi zinamhusisha kuwa kwenye mchakato wa kurejea Atletico Madrid.
Lakini miamba hao wa Ligi ya Hispania wapo tayari kulipa paundi milioni 30 tu, ikiwa ni kudogo zaidi ya paundi milioni 50 walizotoa Chelsea kumsajili mshambuliaji huyo.
Arsenal wapo tayari kumsajili Julian Draxler, na PSG wanataka kiasi cha paundi milioni 32 kukamilisha usajili wa mchezaji huyo majira ya joto, kwa mujibu wa The Times . 

Labels:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

CHARLES CHAMI. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget