http://tropicalpoultryfarming.blogspot.com/

AZAM YASHUKA HADI NAFASI YA 2 BAADA YA KUBANWA MBAVU NA JKT YANAGA YAUWA YAPANDA KILELENI


Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam FC wamekubali kuipisha Yanga kileleni baada ya kabanwa huko mlandizi


Azam FC imetoka sare ya bila kufungana dhidi ya JKT Ruvu katika mechi iliyochezwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi, koani Pwani.

Sare hiyo ya bila mabao, inaifanya Azam FC kufikisha pointi 26 wakati Yanga ambayo imeibuka na ushindi dhidi ya Prisons inafikisha pointi 28.

Azam FC ndiyo iliyokuwa  inaongoza kwa kuwa na pointi 25 sawa na Yanga lakini tofauti ilikuwa ni mabao ya kufunga na kufungwa.

Katika kipindi cha kwanza dakika 15 za kwanza, Azam FC ilishambulia zaidi, lakini washambuliaji wake John Bocco na Kipre Tchetche hawakuwa makini.

Kipindi cha pili, mambo yalibadilika na JKT kutawala huku wakionekana kuwasumbua Azam FC, hata hivyo nao hawakuwa makini kumalizia nafasi walizozipata.
 Mhezo huo uliokuwa wa kiporo ndio wa mwisho wa kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi kuu Tanzania bara.

Labels:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

CHARLES CHAMI. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget