Ligi Kuu England
BPL: MSIMU WAISHA KWA MAGOLI KIBAO, ARSENAL, CHELSEA ZIPO UCL!
>>SPURS KUCHEZA EUROPA LIGI!
>>SIR ALEX AAGWA KWA SARE YA 5-5 NA WBA!!
>>RVP ATWAA BUTI YA DHAHABU!!
BPL, Barclays Premier League, leo imemaliza Msimu wake wa 2012/13 kwa kukamilisha idadi ya Timu 4 za kucheza UCL,UEFA CHAMPIONZ LIGI, Msimu ujao kwa Chelsea na Arsenal kuungana na Mabingwa Manchester United na Manchester City na kuitupa Tottenham kucheza EUROPA LIGI.
Kabla ya Mechi za leo tayari alishapatikana Bingwa ambaye ni Man United na Mshindi wa Pili ni Man City na Timu zilizoshushwa Daraja ni Wigan, QPR na Reading.
Kilichobaki kilikuwa kinyang’anyiro cha Nafasi za 3,4 na 5 ambapo Chelsea imefanikiwa kukamata ya Pili na Arsenal ya 4 hivyo kucheza UCL lakini Chelsea, pamoja na Man United na City, zitacheza Makundi, na Arsenal kuanza hatua ya Raundi ya Mchujo na ikifuzu itaingia Makundi.
Tottenham, kwa kumaliza Nafasi ya 5, itacheza EUROPA LIGI kuanzia Hatua ya Mchujo.!
>>SIR ALEX AAGWA KWA SARE YA 5-5 NA WBA!!
>>RVP ATWAA BUTI YA DHAHABU!!
BPL, Barclays Premier League, leo imemaliza Msimu wake wa 2012/13 kwa kukamilisha idadi ya Timu 4 za kucheza UCL,UEFA CHAMPIONZ LIGI, Msimu ujao kwa Chelsea na Arsenal kuungana na Mabingwa Manchester United na Manchester City na kuitupa Tottenham kucheza EUROPA LIGI.
Kabla ya Mechi za leo tayari alishapatikana Bingwa ambaye ni Man United na Mshindi wa Pili ni Man City na Timu zilizoshushwa Daraja ni Wigan, QPR na Reading.
Kilichobaki kilikuwa kinyang’anyiro cha Nafasi za 3,4 na 5 ambapo Chelsea imefanikiwa kukamata ya Pili na Arsenal ya 4 hivyo kucheza UCL lakini Chelsea, pamoja na Man United na City, zitacheza Makundi, na Arsenal kuanza hatua ya Raundi ya Mchujo na ikifuzu itaingia Makundi.
Tottenham, kwa kumaliza Nafasi ya 5, itacheza EUROPA LIGI kuanzia Hatua ya Mchujo.
Post a Comment