http://tropicalpoultryfarming.blogspot.com/

MERY KEITANY WA KENYA ASHINNDA MBIO ZA NEW YORK MARATHON

Keitany, 34, alitumia muda wa saa mbili, dakika 24 na sekunde 26 na kuwa mwanamke wa kwanza kufanya hivyo tangu raia wa Norway Grete Waitz - aliyeshinda mbio hizo mara tano mtawalia.
"Kushinda mara tatu si rahisi, na ina maana kubwa sana kwangu. Si rahisi lakini nilifanikiwa," amesema.
Bingwa wa dunia kutoka Eritrea Ghirmay Ghebreslassie, 20, alimshinda Mkenya Lucas Rotich mbio za wanaume na kuwa mshindi wa Marathon ya New York mwenye umri mdogo zaidi.
Ghebreslassie, aliyemaliza nambari nne London Marathon na Olimpiki Rio alitumia muda wa 2:07:51 na kuwanyima Wakenya ubingwa wa nne mtawalia katika Marathon kwa wanawake na wanaume.
"Najionea fahari sana kutokana na ushindi wangu, na kwamba mimi ni wa kwanza kutoka nchi yangu kushinda," amesema.
Mmarekani Tatyana McFadden alishinda taji lake la nne mbio za wanawake wa kutumia magurudumu New York akitumia muda wa saa moja dakika 47 na sekunde 43.
Sasa ameshinda mbio 17 kubwa za marathon zilizofanyika karibuni, zikiwemo London, Boston, Chicago na New York.
Chanzo BBC
Labels:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

CHARLES CHAMI. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget