http://tropicalpoultryfarming.blogspot.com/

ashitakiwa kwa Fifa




ETOILE du Sahel ya Tunisia inakusuduia kumshitaki mshambuliaji wake, Emmanuel Okwi katika Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kwa kuingia mitini katika klabu hiyo.
Okwi hajaonekana katika klabu hiyo kwa zaidi ya siku 30, na amekuwa akionekana akirandaranda katika mitaa ya jiji la Kampala, Uganda bila wasiwasi wowote.
Klabu hiyo ilimruhusu Okwi kujiunga na timu yake ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’ katika mechi za kufuzu Kombe la Dunia, lakini tangu wacheze mechi dhidi ya Angola mjini Kampala Juni 15, mwaka huu, mshambuliaji huyo ameshindwa kurejea Tunisia na hajatoa taarifa yoyote.
Etoile du Sahel katika barua waliyomuandikia Okwi Julai 12 mwaka huu (Ijumaa iliyopita) na kusainiwa na Katibu Mkuu, Adel Ghith inasema kuwa iwapo straika huyo angekuwa hajarejea mpaka jana Jumatatu ingempeleka katika  vyombo husika vya sheria kwa hatua zaidi.
Katika barua hiyo, ambayo Mwanaspoti inayo, Katibu Mkuu wa Etoile du Sahel amemwambia Okwi kuwa licha ya kupigiwa simu mara kwa mara na makocha wa klabu hiyo tangu Juni 23, mchezaji huyo ameshindwa kuonyesha ushirikiano wowote.
“Ukiwa kama mchezaji profesheno, matendo yako yanachukuliwa kama kushindwa kuheshimu majukumu yako na ni kwenda kinyume na mkataba wako na klabu,” inasema sehemu ya barua hiyo.
Klabu hiyo imemkumbusha Okwi kuwa mkataba wake wa miaka mitatu utakwisha Julai 15, 2016 na kwamba kwa kutoripoti klabuni hapo ni kwenda kinyume na kifungu cha 2, 8 na 16 cha mkataba wake.
Katibu huyo katika barua hiyo amesema Okwi alikuwa amepewa mpaka jana Jumatatu awe ameripoti katika klabu hiyo vinginevyo atachukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kufikishiwa katika vyombo husika vya kisheria.
Katibu huyo ameandika barua pepe nyingine mwishoni mwa wiki na kumkumbusha Okwi kuwa suala lake litafikishwa katika Shirikisho la Soka Tunisia (FTF) na Fifa.
Shirikisho la Soka la Uganda (Fufa) nalo limemuandika barua Okwi kumuonya kuhusu kitendo hicho.
“Jambo hili lipo ndani ya mamlaka yako na klabu. Fufa tulikuruhusu kuondoka ili urejee katika klabu yako, tunakusihi uheshimu kanuni za Fifa katika suala hili,” inasema barua iliyoandikwa na Katibu Mkuu wa Fufa, Edgar Waston Suubi.
Hata hivyo, habari ambazo Mwanaspoti inazo zinadai kuwa Okwi amegoma kujiunga na klabu yake kwa sababu haijamlipa baadhi ya fedha zake za kusaini pamoja na mshahara wa miezi mitatu.

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

CHARLES CHAMI. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget