http://tropicalpoultryfarming.blogspot.com/

LIGI YA MABINGWA MAN CITY KUIVAA BARCA BILA YA MUNGU WAO YAYA TOURE


Uwanja wa Etihad Jijini Manchester utalipuka kwa mpambano mkali wa Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI kati ya Manchester City na FC Barcelona.
Mechi hii ni Marudio ya Mechi ya Msimu uliopita ya Raundi hii hii ya Mashindano haya wakati Man City ilipotolewa na Barcelona kwa Jumla ya Mabao 4-1 katika Mechi mbili ambazo kila Mechi City ilimaliza Mtu 10 baada ya Mchezaji wao mmoja kupewa Kadi Nyekundu.

Katika Mechi hizo, Barcelona walishinda Mechi ya Kwanza iliyochezwa Etihad Bao 2-0 na
kwenye Marudiano huko Nou Camp, Barca ilishinda Bao 2-1.
Hali za Timu
Man City itamkosa Kiungo wao mahiri Yaya Toure ambae anamalizia Kifungo chake cha Mechi 3 alichopewa na UEFA lakini Straika wao mpya Wilfried Bony ruksa kuanza Mechi hii.
Barcelona huenda wakamchezesha Straika wao Luis Suarez ambae atakuwa akicheza Mechi yake ya kwanza Nchini England tangu aihame Liverpool mwanzoni mwa Msimu.
Tathmini
Man City walishindwa kuvuka hatua ya Makundi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI katika Misimu ya 2011/12 na 2012/13 lakini katika Misimu miwli iliyopita walivuka na kukwamia hatua ya Raundi hii.
Wikiendi iliyopita, Timu zote zilikuwa kwenye Ligi za kwao kwa Barcelona kuchapwa kwao Nou Camp Bao 1-0 na Malaga katika La Liga baada ya kushinda Mechi 11 mfululizo wakati City ikiitwanga Newcastle United Bao 5-0 kwenye Ligi Kuu England.
Timu zote hizo mbili zinashika Nafasi za Pili za Ligi za Nchi zao.
Akiongelea mtanange huu wa Uwanja wa Etihad, Sentahafu wa Barca, Gerard Pique, ambae aliichezea Man United ambao ni Mahasimu wakuwa wa City, alisema: “Hii ni moja ya Gemu ya Mwaka, na ni muhimu kwetu kwa sasa. Watajaribu kutushambulia na hilo linatufaa sisi. Imedhihirishwa kwamba tunakuwa vyema dhidi ya Timu zinazotushambulia kwa sababu tunaweza kupiga kaunta ataki!”
Nae Straika wa Man City, Sergio Aguero, ametamka: “Hii ni Gemu mpya na sisi sasa si sawa na Msimu uliopita na wao pia sivyo!”
Meneja wa City Manuel Pellegrini ameahidi Timu yake itacheza kwa kushambulia tu.

Labels:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

CHARLES CHAMI. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget